Ikulu Kunani? Poem by Abdallah Mpogole

Ikulu Kunani?

Ikulu ni jumba gani? Mbona watu waliota!
Heshima na kitu gani, watu huenda kufata.
Mbio lukuki za nini, kisa mpana ukuta?
Kipi hasa chawavuta, kuitwa jina Rais?

Kikosi hakipanguki, toka enzi ya Hayati.
Vikongwe hawabanduki, wanavutana mashati.
Vijembe vita na chuki, makundi na mikakati.
Ipo biashara gani, Mwalimu aliuliza.

COMMENTS OF THE POEM
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Abdallah Mpogole

Abdallah Mpogole

Iringa, Tanzania
Close
Error Success