Ada Ya Mja Poem by Fadhy Mtanga

Ada Ya Mja

Hili linawezekana, ijapokuwa ni gumu,
Na halitoshindikana, ndiyo yetu majukumu,
Nitakufundisha sana, mi hapa ndiyo mwalimu.

Mimi sishindwi na kitu, sijawahi asilani,
Ncha yangu siyo butu, ina makali fulani,
Mimi ni mtu wa watu, tangia hapo zamani.

Kila kitu ninaweza, hakuna nisichojua,
Haya nayowaeleza, ndivyo itakavyokua,
Haswa nitatekeleza, tena kwa kila hatua.

Mja huongea hivyo, tena kwa kusisitiza,
Huaminika vilivyo, ni fundi wa kueleza,
Vyovyote vile iwavyo, husisitiza aweza.

Leo hivi kesho vile, alimradi maneno,
Tawapiga watu shule, kwa ahadi zake nono,
Mwishowe mbivu wasile, japo wamengoja mno.

COMMENTS OF THE POEM
Dickson Mseti 15 March 2010

hongera tupo pamoja ndugu.

0 0 Reply
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Fadhy Mtanga

Fadhy Mtanga

Dar es Salaam, Tanzania
Close
Error Success