Nchi Yetu Poem by priscah Mutswenje

Nchi Yetu

Nchi yetu Kenya ni rembo, tuipake mafuta
Tuishi kama kitambo, kusiwe navyo vita
Nipende kwa kila jambo, sisi wote twapita
Tumwache hajambo, tusije baki kujuta

Kupokea namba wani, kuishi si kukura
Uraia kweli deni, kulipa nako bora
Tuwe bara au pwani, ni kwazo zetu sera
Twelewe kulikoni, amani kwazo kura

Uraia kufaana, kwa shida na raha
Haja gani kupigana, kinyama bila siha
Twajibike Kenya bana, kwelewa uraia
Nayo mambo yakibanana, upesi kuyatwaa

Tupunguzeni lawama, jamani sijivune
Twataka u usalama, jirani sipigane
Upenda kuutazama, shida tuzikane
Tuutende huu wema, mabaya tuyakane

Uraia si ulafi, ni kupinga utani
Wasilete mali ghafi, kututia unyani
Viongozi ni wasafi, wanaoleta fani
Hatutaki ukorofi, huharibu amani


Mama zetu boresheni, ukulima na hali
Utu nao tufunzeni, tuwe walo tuli
Sote tutafurahini, raia mkijali
Uchumi imarisheni, tupate nazo mali

Watoto tusichoshwe, matusi au ghasia
Twakana tusipotoshwe, mawaidha pasia
Kwa matendo twelimishwe, na tupewe husia
Uraia tuonyeshwe, uje kama masia

Namaliza langu somo, shairi la shauri
Maovuni hapa simo, twabiri lipi gari
Jiulize yaliyomo, kubadili safari
Nafika kwa hiki kikomo, kuomba la kadiri

COMMENTS OF THE POEM
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Close
Error Success