Kutwa, kucha nakuwaza,
japo wewe wanikwaza,
wafanya moyo wangu kudunda,
hata nikachukia kitanda.
Acha kunipa mawazo,
nahitaji lako tulizo,
usibwage wangu moyo,
nikakimbia zangu nyayo.
Fanya hima sichelee,
nijihisi wa pekee,
mwili wangu unenepe,
niachane na mapepe.
Wamoyo wangu Wamoyo,
tupilia mbali choyo,
karibu nami sogea,
nipate cha kuongea.
Wajua tunapendeza,
sina haja kujikweza,
usicheze nami mbali,
punguza yako makali.
hhhhhh kumbe shairi kama hili, latoka wapi bila wewe Grace, kazi nzuri kweli
mahabuba wa moyo uliyemthamini kwa lugha yako mwanana.endelea kuandika dada.
This poem has not been translated into any other language yet.
I would like to translate this poem
Lovely and nice poem keep it up