Hili linawezekana, ijapokuwa ni gumu,
Na halitoshindikana, ndiyo yetu majukumu,
Nitakufundisha sana, mi hapa ndiyo mwalimu.
Mimi sishindwi na kitu, sijawahi asilani,
Ncha yangu siyo butu, ina makali fulani,
Mimi ni mtu wa watu, tangia hapo zamani.
Kila kitu ninaweza, hakuna nisichojua,
Haya nayowaeleza, ndivyo itakavyokua,
Haswa nitatekeleza, tena kwa kila hatua.
Mja huongea hivyo, tena kwa kusisitiza,
Huaminika vilivyo, ni fundi wa kueleza,
Vyovyote vile iwavyo, husisitiza aweza.
Leo hivi kesho vile, alimradi maneno,
Tawapiga watu shule, kwa ahadi zake nono,
Mwishowe mbivu wasile, japo wamengoja mno.
This poem has not been translated into any other language yet.
I would like to translate this poem
hongera tupo pamoja ndugu.