Umepita muda niloahidi,
Hakuna dalili ya kurudi,
Walau salamu,
Ningefanyaje?
Mwanikumbuka?
Au siasa zimewapa ahadi mpya,
Mkasahau yote,
Poa.
Sipo mbali nanyi wenzangu,
Nimetamani nami nirudi,
Niwe hai au mfu,
Mtaona!
Fikra zenu ndilo tukio,
Ninalo litaraji,
Ninazo hazijanitoroka,
Zangu mie.
Fikra zangu zifike kwenu,
Ziwagutushe,
Walolala ziwaambie,
Vukani!
‘Kwa wenye mioyo safi’
This poem has not been translated into any other language yet.
I would like to translate this poem