Mwananchi Mimi Poem by Fadhy Mtanga

Mwananchi Mimi

Umepita muda niloahidi,
Hakuna dalili ya kurudi,
Walau salamu,
Ningefanyaje?

Mwanikumbuka?
Au siasa zimewapa ahadi mpya,
Mkasahau yote,
Poa.

Sipo mbali nanyi wenzangu,
Nimetamani nami nirudi,
Niwe hai au mfu,
Mtaona!

Fikra zenu ndilo tukio,
Ninalo litaraji,
Ninazo hazijanitoroka,
Zangu mie.

Fikra zangu zifike kwenu,
Ziwagutushe,
Walolala ziwaambie,
Vukani!

‘Kwa wenye mioyo safi’

COMMENTS OF THE POEM
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Fadhy Mtanga

Fadhy Mtanga

Dar es Salaam, Tanzania
Close
Error Success