Ukijua jambo jema unijuze ndugu yako...
La kututia nguvu mwili sinifiche ndugu yako...
Kama ni ilmu ya manufaa unifunze ndugu yako...
Sinitenge kwa ulacho hata kidogo sinifishe njaa ndugu yako...
ufanye kwangu na mie nifanye hayo kwako...
Kwa uzima na umauti mie ntakuwa ndugu yako...
Litokealo kwa uwezo wake mola, sie tuwe wastahimilivu...
Nimekukumbuka ndugu yangu, apendapo yeye twaja kuonana tena...
Amani, upendo na utulivu vitawale maisha yako...
This poem has not been translated into any other language yet.
I would like to translate this poem