Utakuwa Wangu Poem by Fadhy Mtanga

Utakuwa Wangu



Jua huipenyeza nuru,
Nuru njema ya asubuhi,
Hupenya ndani ya moyo wangu,
Kuamsha matumaini,
Na hisia mpya.

Moyoni yupo mtu mmoja,
Wa pekee,
Asiye nacho kifani,
Kwa maisha yangu yote,
Humu duniani.

Kwa sababu,
Umeamsha hisia mpya,
Hisia ziujazazo moyo wangu,
Kunipa mawazo,
Huku nikiwa na faraja.

Nimeamini tangu siku ile,
Ya kwanza tulipokutana,
Kuwa kwa hakika,
Utakuwa wangu,
Kwa sababu,
Unastahili hivyo.

COMMENTS OF THE POEM
Steve Vaughan 17 December 2008

What does it mean in english?

0 0 Reply
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Fadhy Mtanga

Fadhy Mtanga

Dar es Salaam, Tanzania
Close
Error Success