Nuru ya jua uamkapo,
Tumaini zaidi liwepo,
Na huzuni ikuondokapo,
Pindi moyo ufarijikapo,
Farijika nami.
Usilemewe sana kichwani,
Moyo siutose majonzini,
Walishasema hapo zamani,
Basi jipe amani moyoni,
Ufurahi nami.
Muda ungeweza rudi tena,
Tungeipenda siku ya jana,
Idumu muda mrefu sana,
Hakika tungefurahiana,
Jiliwaze nami.
Safari ndiyo yetu maisha,
Mwingine yake kakamilisha,
Kipande tulichokibakisha,
Nasi siku moja kitakwisha,
Jiliwaze nami.
Pengo lake huleta majonzi,
Moyo ukajawa na simanzi,
Tukimpa imani Mwenyezi,
Kuwa peke yetu hatuwezi,
Ufurahi nami.
Yahimili hayo maumivu,
Uzidishe ustahimilivu,
Kwa maana Mungu yu na nguvu,
Kuyafanya maisha angavu,
Jiliwaze nami.
This poem has not been translated into any other language yet.
I would like to translate this poem