Wenyewe! Poem by Fadhy Mtanga

Wenyewe!

Wape nafasi waj’amulie,
Na sie tuwasikilizie,
Nini na nini wajipatie,
Ndugu zao wayafaidie,
Vile iwavyo ama isiwe,
Utawafanya nini?

Nadhani sie tuwaachie,
Wanapenda tusiwaambie,
Jirani tusiwasimulie,
Ni bora haya usisikie,
Wala hata yasikuingie,
Utaumiza moyo.

Ngoja huo mwaka ufikie,
Waje hapa ili watwambie,
Ni vipi haya watufanyie,
Walitaka tusiwapigie?
Wanalo lipi tuwasikie?
Mie hata silijui.

Kumekucha mbiu isikie,
Usingizini ikuzindue,
Yale makosa usirudie,
Yanakufanya ugharamie,
Vitu vyao ‘sibabaikie,
Leo vyakutesa!

Kura tena usiwapatie!

COMMENTS OF THE POEM
Luca fwila 24 November 2018

safiiii brooo

0 0 Reply
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Fadhy Mtanga

Fadhy Mtanga

Dar es Salaam, Tanzania
Close
Error Success