Thamaniye Chupi Poem by Abdallah Mpogole

Thamaniye Chupi

Wapo watu na porojo, chupi kutoithamini.
Nalileta kwenu zogo, nijibuni niamini.
chupi thamaniye togo, na ereni sikioni?
Thamani utaijua, siketi wakiivua.

Mwingine alinambia, havai kiso maana.
Akivaa sintojua, Pamoja tutafanana.
Hadhi ya chupi najua, ndo hasa ninapingana.
Thamani utaijua, suruali ikichanwa.

Swali langu la kijinga, majibu mazuri nipe.
Kwa msuli kujifunga, chupi haiwekwi pweke.
Hata wavaao kanga, paso chupi sekeseke.
Thamani utaijua, pale kanga ikilowa.

Tamati nasisitiza, chupi thamaniye kubwa.
Uliza wanolegeza, makalio yanazibwa.
Chupi si ya kubeza, si mtoto si mkubwa.
Thamani utaijua, nguo zote zikiibwa.

POET'S NOTES ABOUT THE POEM
Imefikia msemo miongoni mwa watu ati kwamba chupi kazi yake ni nini, mtu akivaa haionekani au asipovaa pia haionekani, hivyo basi nikaona ni bora niwajuze/ tujuzane na watu wengine kwa kile mie ninachoelewa juu ya thamani ya chupi kama vazi.
COMMENTS OF THE POEM
Linet Sabastian 06 December 2016

Umeandika na kuchambua vyema.

0 0 Reply
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Abdallah Mpogole

Abdallah Mpogole

Iringa, Tanzania
Close
Error Success